Dhana.
Ni
hali ya kuweka vielelezo katika mazingira sahihi na yaliyo mazuri au salama ili
kuhifadhi kutokana na uharibifu wa aina yoyote ule.
Waharibifu wa vielelezo.
Waharifu
wa vielelezo vya kufundishia/ kujifunzia ni wengi ikiwa ni pamoja na mikono ya
watu wenyewe. Waharibifu wengine ni hali ya hewa, upepo, vumbi, wadudu
waharibifu n. k.
Hali
ya hewa
Ni
moja kati ya waharibifu wa zana au vifaa vya kufundishia na kujifunzia. Athari
zinazosababishwa na hali ya hewa ni kubabuka rangi kwa chati au picha
inapobandikwa kwa muda mrefu hupoteza nuru ya rangi.
Aidha
hali ya hewa baridi husababisha ukungu kwenye vifaa ambavyo havikuhifadhiwa
vizuri mfano kanda za video, kanda za kinasa sauti n. k.
Hivyo basi mara baada ya kutumika mwalimu anatakiwa kuvihifadhi ili
visiharibike.
Upepo
na vumbi
Upepo
unapeperusha chati na picha zilizopachikwa ukutani na juu ya ubao husababisha
kuchanika. Upepo pia hupeperusha vumbi ambalo huaribu vitu kama
vide, redio, kanda za sauti n. k. Iwapo
vifaa hivi havikuhifadhiwa vizuri vinaweza kuharibika.
Wadudu
waharibifu
Mfano
mchwa, mende, panya n.k.Mwalimu
analazimika awe muangalifu sana juu ya wadudu hawa
kwani ni wadudu hatari sana
kwa kuharibu zana za kufundishia.
NJIA ZA UTUNZAJI WA VIELELEZO NA TEKNOLOJIA
Katika
utunzaji wa vielelezo na teknolojia kwa kufundishia/ kujifunzia. Vielelezo
vinaweza kugawanyika katika makundi mawili (2)
(i)
Vinavyowekeka
kwa muda mrefu
(ii)
Vinavyowekeka
kwa muda mfupi
Vinavyowekeka
kwa muda mfupi ni kama:- matunda, dagaa, aina mbalimbali za mboga za majani,
hizi hutumika kwa muda mfupi na kutupwa jalalani na vile vinavyowekeka kwa muda
mrefu, viwekwe kwa utaratibu mzuri ili visiharibike
Njia
zifuatazo zinaweza kutumika katika kuhifadhi vielelezo:-
(i)
kuhifadhi
katika visanduku au masanduku maalumu.
(ii)
Kuviweka
katika kabati kutokana na wadudu waharibifu
(iii)
Kuviweka
katika mifuko ya plastiki na kufungwa vizuri ili hewa isipite ambayo hatimaye
huenda ikasababisha uharibifu
(iv)
Kutumia
mikebe isiyopenyeza hewa. Hii inaweza kuhifadhi lenzi za projekta au projekta
yenyewe na vitu vidogovidogo vinavyoharibika kwa ukungu vihifadhiwe katika
mikebe hiyo au katika mikoba yao
(v)
Kuvisafisha
na kuviangalia mara kwa mara
(vi)
Njia
ya kugandishwa kwenye karatasi ngumu na kufanya fremu kwa mfano chati au picha
zilizochorwa kwenye karatasi nyepesi zinaweza kubandikwa, kuninginizwa juu ya
ukuta wa darasa
(vii)
Kuviweka
katika chumba maalumu.
(viii)
Vipangwe
vizuri ili visigongane au kujeruhiana.