WELCOME NOTE

WELCOME NOTE

PICHA

PICHA

TANGAZO

Monday, September 3, 2012

MAELEZO KWA UFUPI KUHUSIANA NA SOMO LA VIELELEZO NA TEKNOLOJIA


Vielelezo  na  Teknolojia  kama  somo  linalojitegemea,  linamlen ga  mkufunzi  ili  aweze kuwawezesha  wanachuo  kupata  ujuzi  na  stadi  za  kubuni,  kufaragu a,  kutengeneza  na kutumia  zana  au  vifaa  na  teknolojia  asilia  na  ile  ya  kisasa  katika  kufundishia  na kujifunzia.

Lengo  KUU la somo hili  ni  kuwaanda  wanachuo   wa  ualimu  wa  elimu  ya  msingi  ngazi  ya  cheti  waweze  kujifunza  na  kufundisha masomo mbalimbali kwa kutumia zana zilizofaraguliwa au kutengenezwa.
Hapo  awali,  somo  la  Vielelezo  na  Teknolojia  lilikuwa  halifundishwi  chuoni  kama somo  linalojitegemea. Badala  yake  wakufunzi  wa  kila  somo  walikuwa  wakitoa maelekezo  ambayo  hayakumwezesha  mwanachuo  kuandaa  zana  au  vifaa  vya kufundishia. Mara nyingi  maelekezo  hayo  hayakuzingatia  maarifa,  stadi,  ujuzi  na uwezo wa mwanachuo.
Somo hili litamwezesha  mwanachuo  wa  ualimu elimu ya msingi ngazi ya cheti  kupata ujuzi,  maarifa,  stadi,  uwezo  na  mbinu  mbalimbali  za  kubuni,  kufaragua  na kutengeneza zana au vif aa bora kwa ajili ya  kumwezesha kufundisha kwa ufanisi.
Katika  somo  hili,  Vielelezo  na  Teknolojia  asilia  ina  maana  ya  zana  na  vifaa  rahisi ambavyo  huweza  kupatikana  au  kutengenezwa  katika  mazingira  alimo  mwalimu  na
wanafunzi  kwa  kutumia  makunzi  yaliyomo  katika  mazingira  hayo.    Vitu  vingi  halisi huweza  kupatikana  kwenye  mazingira  tulimo  kama  vile  matunda,  samani,  mimea,viumbe  hai  na  vingine  vingi.Vifani  vya  maumbo  mbalimbali  pia  huweza
kutengenezwa  katika  mazingira  kama  vile  vifani  vya  viumbe  hai,  maumbo  yenye ukumbi kama vile mche duara, mche mstatili, tufe na vingine vin gi.Kwa upande  mwingine  ‘Vielelezo na Teknolojia    kisasa  ‘ina maana  ya  zana au vifaa
vya  kisasa  ambavyo  ni  vigeni  na  havijazoeleka  katika  kuvitengeneza  au  kuvitumia.
Zan a au vifaa hivi ni kama vile  matumizi  ya  video, luninga, filamu  na ko mpyuta.  
 Mkufunzi  unashauriwa  kuwa unapoongoza  shu ghuli  za  kujifunzia ni vema ufikirie na kuzingatia  masuala  mtambuko.Mathalani  uzingatie  jinsia  kwenye  shughuli zinazohusu  vikundi  vya  kujifunza,usafi  na  utunzaji  wa  mazingira  kabla  na  baada  ya somo.Pia, zana  au vifaa  vitakavyobuniwa,  kufaraguliwa, au kutengenezwa vihusishe
masuala  ya  afya  au magonjwa kama vile  Malaria,  UKIMWI  na mengineyo kwa  kadri itakavyoonekana inafaa au kukidhi haja ya somo husika.

No comments:

Post a Comment